Jumatano, 25 Februari 2026

VITA DHIDI YA MAJIBU YAKO

 MTUNZI: REV.AMOS

SIMU/WHATSAPP: +255759199463


SOMO:

VITA DHIDI YA MAJIBU YAKO.

➖ Mpendwa kupokea majibu ya MUNGU maishani kuna vita katika ulimwengu wa Roho.

➖Mara nyingi Adui anakutegea kwenye wakati wako wa kupokea.

➖Adui anakuwekea vizuizi katika ulimwengu wa Roho ili usipokee, KATAA KWA JINA LA YESU.

➖MUNGU ANATUWAZIA MEMA.

👇👇👇👇👇

YEREMIA 29:11-12

[11]Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema BWANA, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho. 


[12]Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.


➖ Katika mapito yote, ukimlilia MUNGU yeye anasikia.

👇👇👇👇

KUTOKA 22:23

[23]Ukiwatesa watu hao katika neno lo lote, nao wakanililia mimi, hakika yangu nitasikia kilio chao,


➖MAJIBU YA DANIEL YALIKUTANA NA VITA KUBWA.

👇👇👇👇

DANIEL 10:11-13

[11]Akaniambia, Ee Danieli, mtu upendwaye sana, yafahamu maneno nikuambiayo, ukasimame kiwima-wima; maana kwako nimetumwa sasa. Na aliponiambia neno hili, nalisimama nikitetemeka. 


[12]Ndipo akaniambia, Usiogope, Danieli; kwa maana tangu siku ile ya kwanza ulipotia moyo wako ufahamu, na kujinyenyekeza mbele za Mungu wako, maneno yako yalisikiwa; nami nimekuja kwa ajili ya maneno yako. 


[13]Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga siku ishirini na moja; bali, tazama, huyo Mikaeli, mmoja wa hao wakuu wa mbele, akaja kunisaidia; nami nikamwacha huko pamoja na wafalme wa Uajemi.


➖ Mpendwa, komboa wakati wako wa kupokea.

➖Kuna Adui amekutegea siku ya kujifungua kwako, Siku ya kuanza KAZI katika Ofisi hiyo, Siku ya malipo yako n.k

➖KATAA MAJIBU YAKO KUCHELEWA.

➖VUNJA ROHO ZA VIZUIZI KATIKA MAISHA YAKO.

➖OMBA MUNGU AKUTUMIE MALAIKA WA KUKULETEA MAJIBU.


Barikiwa!!!


___________ Mwisho ___________

E-mail: pasteronesmo@gmail.com

+255759199463

+255625313609

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni