Alhamisi, 5 Machi 2026

YESU NI SULUHISHO

 MTUNZI: REV.AMOS

SIMU/WHATSAPP: +255759199463

SOMO:

YESU NI SULUHISHO.

👇👇👇👇

 *MAOMBOLEZO 3:25* 

"BWANA ni mwema kwa hao wamngojeao, 

Kwa hiyo nafsi imtafutayo"

➡️Yesu ni MWEMA maishani mwetu.


➖Maisha ya mwanadamu yana changamoto nyingi zinazohitaji ufumbuzi.

➖Yesu huleta ufumbuzi wa changamoto za Maisha yetu.

➖Uwepo wa Yesu katika maisha yako ni ufumbuzi wa changamoto zako.

➖Mpe nafasi Yesu afanyike SULUHISHO.

➖Pale akili yako inapofika mwisho ndipo Neema ya MUNGU inapojidhihirisha kwako.

➖YESU NI SULUHISHO LA SHIDA YAKO, MPE NAFASI NA FUATA MAELEKEZO.

➖Uwepo wa Yesu katika Arusi ya KANA ulileta SULUHISHO LA DIVAI ILIPOISHA.

👇👇👇👇👇

*YOHANA 2:1-10* 

[1]Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo. 


[2]Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake. 


[3]Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai. 


[4]Yesu akamwambia, Mama, tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia. 


[5]Mamaye akawaambia watumishi, Lo lote atakalowaambia, fanyeni. 


[6]Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata kadiri ya nzio mbili tatu. 


[7]Yesu akawaambia, Jalizeni mabalasi maji. Nao wakayajaliza hata juu. 


[8]Akawaambia, Sasa tekeni, mkampelekee mkuu wa meza. Wakapeleka. 


[9]Naye mkuu wa meza alipoyaonja yale maji yaliyopata kuwa divai, (wala asijue ilikotoka, lakini watumishi walijua, wale walioyateka yale maji), yule mkuu wa meza alimwita bwana arusi, 


[10]akamwambia, Kila mtu kwanza huandaa divai iliyo njema; hata watu wakiisha kunywa sana ndipo huleta iliyo dhaifu; wewe umeiweka divai iliyo njema hata sasa.


➖Fuata maelekezo ya Yesu afanyike SULUHISHO.

➖Mama wa Yesu (Mariam), aliwaeleza watu wafuate maelekezo atakayoyatoa Yesu ili kupata SULUHISHO LA DIVAI, nami nasema FUATA MAELEKEZO 

➖YESU YUKO KARIBU YETU 

👇👇👇👇

*YEREMIA 23:23* 

[23]Mimi ni Mungu aliye karibu, asema BWANA, mimi si Mungu aliye mbali.


___________ Mwisho ___________

E-mail: pasteronesmo@gmail.com

+255759199463

+255625313609