Jumanne, 5 Agosti 2025

USITENDE DHAMBI TENA

 MWL: REV.AMOS 

CONT: 0759199463

WHATSAPP: +255625313609

E-MAIL: pasteronesmo@gmail.com 


SOMO: USITENDE DHAMBI TENA. 


Yohana 5:14 

"Baada ya hayo Yesu akamkuta ndani ya hekalu, akamwambia, Angalia, umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi"


➖Usitende dhambi yasije kukupata yaliyo mabaya zaidi

➖Umevuka salama, endelea kunyenyekea usitende dhambi tena. 


➖Tunza utakatifu ili Mungu akutendee zaidi na zaidi.


➖Umepata kazi, umeoa, umeolewa, umeinuliwa, umeponywa ugonjwa n.k endelea kutunza utakatifu. 


➖Dhambi inatoa nafasi mapepo kukurudia na kukutesa.

👇👇👇

Luka 11

24 Pepo mchafu amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika; asipoona, husema,


25 Nitairudia nyumba yangu niliyotoka.


26 Hata afikapo, akaiona imefagiwa na kupambwa, ndipo huenda akachukua pepo wengine saba, walio waovu kuliko yeye mwenyewe, wakaingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza.


➖Dhambi inakufanya umilikiwe na Ibilisi. 

👇👇👇

1 Yohana 3:8 

"atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi"


...................MWISHO......................

REV. AMOS 0625313609