Jumanne, 7 Oktoba 2025

MOTO WA INJILI - KARIBU 0759199463 WHATSAPP +255625313609















































 

*KUFUNGULIWA MASIKIO YA KIROHO*

 MWL: REV.AMOS

CONT: +255625313609

E-MAIL: pasteronesmo@gmail.com


SOMO: 

*KUFUNGULIWA MASIKIO YA KIROHO* 


✳️ *Masikio* 

➖ Ni mlango wa fahamu kwa kiumbe hai unaotumika kusikia.

➖Kama yapo masikio ya Ki-Mwili basi tambua yapo na masikio ya kiroho.

➖Masikio yako yafunguliwe kwa jina la Yesu ili uweze kumsikia Mungu lile alitakalo kwako.

👇👇👇

Adamu na Eva walimsikia Mungu.


 *MWANZO 3:8* 

"Kisha wakasikia sauti ya BWANA Mungu, akitembea bustanini wakati wa jua kupunga; Adamu na mkewe wakajificha kati ya miti ya bustani, BWANA Mungu asiwaone"


➖Masikio ya mtu yakifungwa hawezi kumsikia Mungu na hawezi kupokea maelekezo ya Mungu kwake.

 *➖KATAA KUWA KIZIWI WA KIROHO* .

👇👇

 *ISAYA 43:8* 

"Walete vipofu walio na macho, na viziwi walio na masikio"


 *MATHAYO 13:13-15* 

"[13]Kwa sababu hii nasema nao kwa mifano; kwa kuwa wakitazama hawaoni, na wakisikia hawasikii, wala kuelewa. 


[14]Na neno la nabii Isaya linatimia kwao, likisema, 

Kusikia mtasikia, wala hamtaelewa; 

Kutazama mtatazama, wala hamtaona. 


[15]Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, 

Na kwa masikio yao hawasikii vema, 

Na macho yao wameyafumba; 

Wasije wakaona kwa macho yao, 

Wakasikia kwa masikio yao, 

Wakaelewa kwa mioyo yao, 

Wakaongoka, nikawaponya"


 *EZEKIEL 12:2* 

"Mwanadamu, wewe unakaa kati ya nyumba iliyoasi, watu ambao wana macho ya kuona, ila hawaoni, wana masikio ya kusikia, ila hawasikii; kwa maana ni nyumba iliyoasi"


➖Nyakati tulizonazo ni za mwisho ambazo watu wengi hawataki kumsikia Mungu wala kuyasikia mafundisho yake ya kweli.

👇👇

 *2 TIMOTHEO 4:3-4* 

[3]Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima; ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia waalimu makundi makundi, kwa kuwa wana masikio ya utafiti; 


[4]nao watajiepusha wasisikie yaliyo kweli, na kuzigeukia hadithi za uongo.


 *HITIMISHO* 

Omba kufunguliwa Masikio yako ya Kiroho ili umsikie Mungu.


-------------END------------

REV.AMOS

+255625313609

+255759199463

pasteronesmo@gmail.com

INJILI VIJIJINI INAENDELEA - KARIBU KWA SUPPORT M-PESA 0759199463